Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwalimu wa madrasa Dar kizimbani kwa tuhuma za ubakaji

72463 Ubakaji+pic

Thu, 22 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mwalimu wa madrasa, Mussa Juma Musa (26) amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni kwa tuhuma za ubakaji.

Musa ambaye ni mkazi wa Kinondoni amefikishwa mahakamani hapo jana Jumatano Agosti 21, 2019 kujibu shtaka la kumbaka Leila Moses (22).

Akisomewa hati mashtaka  mbele ya hakimu mkazi Caroline Kiliwa,  wakili wa serikali Benson Mwaitenda amedai mtuhumiwa alitenda kosa hilo kati ya Oktoba 2018 na Machi 2019 eneo la  Mwananyamala.

Mshtakiwa alikana shtaka hilo lakini aliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti.

Hakimu Kiliwa amemtaka  mtuhumiwa kutosafiri  bila hati ya mahakama, kuahirisha kesi hiyo hadi   Septemba 18, 2019.

Wakati huohuo, Gabriel Dossa na John Charles walifikishwa mahakamani hapo kwa wizi na uhujumu uchumi wa zaidi ya Sh89 milioni.

Pia Soma

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi na kuingilia miundombinu ya kutolea huduma ya Shirika la Simu Tanzania (TTCL) na kulisababishia shirika hilo hasara ya Sh89 milioni.

Mbele ya hakimu Frank Mushi, wakili wa Serikali Yussuf Aboud amedai Dossa alitenda kosa hilo Julai 24, 2019 eneo la Kawe (triple 7) wilayani Kinondoni.

Anadaiwa kuiba kebo za Sh47 milioni  kinyume na sheria na kuisababishia hasara mamlaka husika.

Charles anadaiwa kutenda kosa hilo Julai 29 ,2019 maeneo tofauti jijini Dar es Salaam na kusababisha hasara ya Sh42 milioni. 

Wakili Aboud amesema watuhumiwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kuingilia miundombinu ya kutolea huduma katika jamii.

Kutokana na kutotimiza masharti ya dhamana watuhumiwa walirejeshwa rumande na kesi hiyo kuahirishwa hadi Septemba 4, 2019.

Chanzo: mwananchi.co.tz