Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwalimu kizimbani tuhuma kupokea rushwa 600,000/-

Dom Taku 0 Mwalimu kizimbani tuhuma kupokea rushwa 600,000/-

Tue, 20 Jul 2021 Chanzo: ippmedia.com

Saveli ambaye ni Kaimu Mtendaji wa Kijiji cha Ilangali wilayani humo, alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma kwa madai ya kutomchukulia hatua mwanafunzi wa darasa la nne.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Dodoma, Sosthenes Kibwengo, mtuhumiwa huyo aliomba rushwa ya Sh.600,000 na kupokea Sh. 400,000 kutoka kwa mtoa taarifa ili asimchukulie hatua mwanafunzi huyo kwa kitendo cha utoro wa mtoto.

Kibwengo alisema kitendo cha mwalimu kudiriki kuomba na kupokea rushwa ni kwenda kinyume cha taaluma yake kwa kukwamisha elimu badala ya kuchochea elimu.

Alisema mtuhumiwa huyo amefunguliwa mashtaka mawili ya kushawishi na kupokea rushwa kinyume cha Kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya 2019.

Mkuu huyo alisema elimu ni ufunguo wa maisha na serikali kila kukicha inasisitiza kuwekeza zaidi katika elimu ikiwamo kuimarisha mazingira ya utoaji elimu.

Chanzo: ippmedia.com