Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia Mwalimu wa Sekondari ya Mkolani, Deogratius Kisandu kwa makosa ya kutumia vibaya mitandao ya kijamii (Cyber Crime) kwa kuandika matusi.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kutumia ukurasa wake wa Facebook kuandika matusi kwa takriban wiki nzima.
Posti zake mbili za mwisho kwenye ukurasa wake wa Facebook alitolea maelezo ya kukamatwa kwa Nabii Tito na kujitabilia kukamatwa na Jeshi la polisi.
“Biblia inakubali kunywa pombe. Nabii Tito yuko sahihi dini ni jambo la hiari na si la Kiserikali. Katiba ya TZ ibara 19. Kunywa Pombe kanisani hakuna kosa mbona Yesu na waasisi wa agano la kale walikunywa Pombe (mivonyo na Divai) mpaka wakalewa….Nabii Tito yuko sahihi, kama wewe unakwazwa anzisha kanisa lako.“ameandika mtuhumiwa Deogratius Kisandu na kwenye posti ya pili alijitabilia kukamatwa na polisi.
“Ku***ba ni haki yangu ya kikatiba ya ibara ya 16 (unyumba). Imeagizwa niwekewe Jeshi au nipigwe pingu kwa kukosa maadili na pia kufukuzwa kazi kisa nataka ku***ba.(MLAANIWEE kabisa, siwezi ishi bila ku***ba).” MUNGU uwasamehe watakao nipiga PINGU maana hawajui NYE*E zinavyonikabili”. AMEEEN”