Bukoba. Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba imemhukumu kunyongwa hadi kufa, mwalimu Respicius Mutazangira baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mwanafunzi wa darasa la tano Shule ya Msingi Kibeta, Sperius Eradius mwishoni mwa mwaka 2018.
Wakati Respicius akihukumiwa kunyongwa, mwalimu mwenzake ambaye alishtakiwa naye, Heriet Gerald ameachiwa huru.
Hukumu hiyo imetolewa leo na Jaji Lameck Mlacha ambaye alisikiliza kesi hiyo kwa mwezi mmoja.
Katika kesi hiyo ilidaiwa kuwa walimu hao walitenda kosa la kumuadhibu kwa kipigo Sperius kwa madai kuwa aliiba mkoba wa mwalimu Eliet ukiwa na fedha.
Endelea kufuatilia zaidi kupata undani wa kinachojiri mahakamani
Soma zaidi: Kusuka au kunyoa leo kesi ya walimu walioshtakiwa kumuua mwanafunzi
Soma zaidi: Mauaji ya mwanafunzi, mtuhimiwa atumia dakika tatu kusoma mistari ya Biblia