Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwalimu Mkuu adaiwa kumbaka, kulawiti mwanafunzi Bunda

Mwalimu Mkuu Adaiwa Kumbaka, Kulawiti Mwanafunzi Bunda Mwalimu Mkuu adaiwa kumbaka, kulawiti mwanafunzi Bunda

Wed, 13 Mar 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linamshikilia mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Masaunga wilayani Bunda, Vicent Nkunguu (39) kwa tuhuma za kumbaka na kumlawiti mwanafunzi wa darasa la sita shuleni hapo kisha kumnywesha sumu.

Akizungumza na Mwananchi kwa simu leo Machi 13, 2024, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Salum Morcase amesema vitendo vya ubakaji na ulawiti vilifanyika siku moja kabla ya kunyweshwa sumu siku iliyofuata lengo likiwa ni kupoteza ushahidi.

Kamanda Morcase amesema mwanafunzi huyo (16) alibakwa Machi 8, 2024 usiku akiwa amelala nyumbani kwa mtuhumiwa huyo Kijiji cha Kisorya alipokuwa amekwenda kwa ajili ya kuwapikia watoto wa mtuhumiwa baada ya kuombwa na mke wa mwalimu huyo aliyesafiri kwenda kwenye maombi katika Kijiji cha Igundu.

"Akiwa amelala na watoto chumbani, mwalimu huyo alikwenda kwenye chumba cha watoto na kumwambia mwanafunzi huyo kuwa, amekosa usingizi na kwenda naye kwenye chumba chake ambako alimbaka na kumlawiti," amesema.

Kamanda Morcase amesema baada ya kumaliza haja zake alimruhusu kurudi chumbani kwa watoto na siku iliyofuata mtoto huyo aliitwa na mama yake kwenda kufukuza ndege kwenye shamba lao la mpunga.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live