Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Muuguzi aua watoto wachanga 10 kwa sumu hospitalini

Srgethryna Muuguzi aua watoto wachanga 10 kwa sumu hospitalini

Tue, 11 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Lucy Letby ameshtakiwa kwa mauaji ya watoto watano wa kiume na wakike wawili.

"Mtoaji sumu alikuwa kazini" katika hospitali ambapo kulikuwa na "kuongezeka kwa kiasi kikubwa" kwa idadi ya watoto wenye afya wanaokufa, mahakama imeelezwa.

Lucy Letby ameshtakiwa kwa mauaji ya watoto watano wa kiume na wakike wawili, na kujaribu kuwaua watoto wengine 10 katika hospitali ya Countess of Chester, Uingereza

Nick Johnson KC, anayeendesha mashtaka, alisema alikuwa "mwenye ukatili wa mara kwa mara" katika kitengo cha watoto wachanga cha hospitali hiyo.

Bi Letby, 32, wa Hereford, anakanusha mashtaka 22 katika mahakama ya Crown ya Manchester.

Akifungua mashtaka, Bw Johnson alisema taasisi hiyo ya Chester ni "hospitali kuu yenye shughuli nyingi... kama nyingine nyingi nchini Uingereza". Hata hivyo, alisema kuwa "tofauti na hospitali nyingine nyingi... ndani ya kitengo cha watoto wachanga katika Hospitali ya Countess ya Chester, mtoa sumu alikuwa kazini".

"Kabla ya Januari 2015, takwimu za vifo vya watoto wachanga katika kitengo cha watoto wachanga katika kituo cha Countess of Chester zililinganishwa na vitengo vingine kama hivyo," alisema.

"Hata hivyo, katika muda wa miezi 18 hivi iliyofuata, kulikuwa na ongezeko kubwa la idadi ya watoto waliokuwa wakifa .''

Alisema ongezeko hilo liligunduliwa na washauri wa hospitali, ambao walikuwa na wasiwasi kwamba "watoto wachanga waliokuwa wakifa wamedhoofika bila kutarajiwa"

"Baada ya kutafuta sababu, ambayo hawakuweza kupata, washauri waligundua kuwa kuanguka na vifo visivyoelezeka vilikuwa na vyanzo vya aina moja," alisema.

"Kuwepo kwa mmoja wa wauguzi wa watoto wachanga na muuguzi huyo alikuwa Lucy Letby." Bw Johnson aliiambia mahakama kwamba kwa vile madaktari hawakuweza kutoa maelezo kuhusu vifo hivyo, polisi waliitwa na kufanya uchunguzi wa kina.

"Tathmini hiyo inapendekeza katika kipindi cha kati ya 2015 na katikati ya 2016, mtu fulani katika kitengo cha watoto wachanga aliwatia sumu watoto wawili ," alisema.

"Upande wa mashtaka unasema hitimisho pekee linalofaa kutolewa kutokana na ushahidi utakaosikia ni kwamba mtu fulani aliwapa insulini watoto hawa kwa makusudi."

"Lucy Leby alikuwa zamu wakati wote wawili walipopewa sumu na tunashuku kuwa yeye ndiye aliyeweka sumu," Bw Johnson alisema. Alisema vifo havikuwa "ajali" na sio "vya ya asili". "Matukio mengi katika kesi hii yalitokea wakati wa zamu za usiku," alisema.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live