Fri, 11 Oct 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dodoma. Martin Temu (33), mtunza fedha wa Benki ya Exim tawi la Dodoma anashikiliwa na polisi kwa madai ya kuiba Sh120 milioni.
Akizungumza leo Ijumaa Oktoba 11, 2019 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema mtuhumiwa ni mkazi wa Dodoma, alipoiba fedha hizo alitoroka.
Amesema msako ulifanyika na alikamatwa mkoani Singida katika nyumba ya kulala wageni.
"Tulimkamata akiwa na Sh37.5 milioni kati ya fedha alizoiba, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili,” amesema Muroto.
Chanzo: mwananchi.co.tz