Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtumishi alieiba dawa za Milioni 88 afukuzwa kazi

Quercetina Substanta Pe Care Toti Romanii Trebuie Sa O Consume Iarna. Ce Este Ea De Fapt 1 660x400.j Mtumishi alieiba dawa za Milioni 88 afukuzwa kazi

Sun, 23 May 2021 Chanzo: millardayo.com

Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza, imewafukuza kazi watumishi wawili baada ya kutiwa hatiani na Mahakama kwa wizi wa dawa katika hospitali ya Wilaya hiyo zenye thamani ya Milioni 88 pamoja na kupokea rushwa zaidi ya Shilingi 100,000.

Akiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya tatu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Joshua Manumbu, amesema kuwa watumishi waliofukuzwa kazi ni pamoja na aliyekuwa Mtumishi wa Maabara katika hospitali hiyo Baraka Bima, ambae alikiri Mahakamani kuhusika na wizi wa dawa hizo na Mtendaji wa Kijiji cha Bukonyo Sabato Mashauri, aliyepatikana na kosa la kuomba rushwa kiasi cha shilingi laki moja na elfu hamsini.

MTOTO JASIRI ANATANGAZA DW, AWASHANGAZA WENGI, ANA UWEZO WA AJABU, AJIZOLEA UMAARUFU MKUBWA DUNIANI

Chanzo: millardayo.com