Dar es Salaam. Mtoto wa miaka minne anayeishi Tabata Mawenzi Paulo Mgaya ambaye taarifa zake zilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba amepotea, jana amepatikana akiwa hai.
Akizungumza na Mwananchi leo mzazi wa mtoto huyo Jimson Mgaya amesema kwamba mtoto wake aliyekuwa amepotea ghafla nyumbani kwao Tabata jioni saa 12 katika mazingira ya kutatanisha alikutwa na wasamaria wema Tabata Chang’ombe saa tatu usiku.
Amesema wasamaria wema walioona ujumbe kwenye mitandao ya kijamii ambapo aliweka picha ya mtoto pamoja na namba za simu walimpigia na kumfahamisha kwamba wamemuona akilia.
“Walinipigia simu wakisema kwamba wamemuona analia na baada ya kumuuliza anatokea wapi hakuweza kujieleza hivyo wakaamua kumpeleka kwa mjumbe wa eneo hilo.
“Mimi nimefurahi jitihada za majirani na watu wanaosoma mitandao ya kijamii kwa kutoa msaada wa kupatikana mwanangu,’’amesema
Amewataka wazazi kuwa makini na watoto wao kwa sababu hata yeye hajui kitu kilichomkuta mtoto wake huyo,kwamba ni mtu aliyemchukua akamwacha huko (Tabata) au ni mtu wa aina