Kamanda wa Polisi, Ramadhan Kingai, ameeleza kuwa wamepata taarifa za mwili wa Blandina kutupwa mbele ya baa ya Maryland majira ya saa tano usiku akiwa tayari amefariki.
Amesema gari aina ya Toyota Noah ilifika katika eneo hilo na kusimama kwa muda mfupi kabla ya kutupa mwili wa Blandina.
Kamanda Kingai ameeleza kuwa bodaboda waliokuwa wamepaki jirani na eneo hilo walishuhudia gari lililowashaa taa likisimama kwa dakika mbili kisha wakaona mwanamke ametupwa.
“Uchunguzi unaendelea ila tulichobaini huyu mtu hakuuliwa pale, mauaji yalifanyika sehemu nyingine pale walienda kumtupa” amesema Kamanda Kingai.