Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mstaafu auawa kikatili Dar

36657 Pic+mstaafu Mstaafu auawa kikatili Dar

Wed, 16 Jan 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Tunsume Sakajinga (60), mkazi wa wilayani Temeke jijini Dar es Salaam ameuawa baada kupigwa na kitu kizito kichwani kisha kuchomwa na mkasi shingoni na mtu anayedaiwa kuwa kijana wake wa kazi za nyumbani.

Msemaji wa familia ambaye ni kaka wa marehemu, Kisa Mwankusye amelieleza Mwananchi kuwa mauaji hayo yametokea juzi Januari 12, 2019 saa tano asubuhi na kwamba marehemu alikutwa amechomwa mkasi shingoni na kupigwa na kitu kizito kichwani.

“Tulipata taarifa hizo saa tano asubuhi, jambo hili linaumiza sana kwa sababu lipo chini ya mikono ya polisi tunawaachia wao,” amesema Mwankusye.

Amesema dada yake alistaafu Desemba 31, 2018 na kwamba nyumbani alikuwa akiishi na kijana huyo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Temeke,  Emmanuel Lukula amethibitisha kuwapo kwa tukio hilo lakini amesema bado wanafanya uchunguzi kubaini nani alihusika na kwamba hakuna mwenye uhakika kama aliuawa na mvulana wake wa kazi.

“Hilo bado tunachunguza na hakuna mwenye uhakika kama ‘houseboy’ wake ndiye alimuua. Siwezi kuthibitisha ila bado tunachunguza,” amesema.



Chanzo: mwananchi.co.tz