Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msiba wakwamisha kesi ya Malinzi na wenzake

70150 Malinzi+pic

Tue, 6 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi  na wenzake  wameshindwa kuanza kujitetea kutokana na Wakili wa utetezi, Richard  Rweyeongeza kufiwa na mkwe wake.

Mbali na Malinzi, washtakiwa wengine ni aliyekuwa Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine, mhasibu wa shirikisho hilo, Nsiande Mwanga na karani Flora Rauya

Wakili wa Takukuru, Leonard Swai ameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  leo Jumanne Agosti 6, 2019 kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kusikiliza upande wa utetezi .

Baada ya maelezo hayo wakili wa utetezi,  Richard Rweyeongeza amedai kuwa amefiwa na mkwe wake maiti ipo nyumbani, hawezi kuendelea na utetezi licha ya kukiri kumuandaa mshtakiwa wa kwanza ambaye ni Malinzi.

"Nina msiba maiti ipo ndani kwangu sitaweza kuendelea na utetezi hivyo ninaiomba Mahakama hii iahirishe shauri hili hadi wiki ijayo," amedai Rweyeongeza.

Hakimu Mkazi Mkuu, Maira Kasonde aliahirisha shauri hilo hadi Agosti 13, 2019 itakapokuja kwa ajili ya Malinzi kujitetea.

Pia Soma

Katika kesi ya msingi Malinzi na wenzake  wanakabiliwa na mashitaka 28, ikiwemo ya utakatishaji fedha ambazo ni Dola za Marekani  375,418.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz