Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mshtakiwa kesi ya mawakala 10 wa TTCL ahoji upelelezi kutokamilika

Mon, 20 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Fabian Ishengoma, mshtakiwa kwa kwanza katika kesi ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu inayowakabili mawakala 10 wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), ameuomba upande wa mashtaka kueleza ulipofikia upelelezi wa kesi hiyo.

Mshtakiwa huyo ameeleza hayo leo Jumatatu Mei 20, 2019 katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi,  Maira Kasonde baada ya wakili wa Serikali,  Janet Magoho kueleza jalada la shauri hilo lipo kwa mwanasheria kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

"Wiki mbili zilizopita tuliambiwa jalada liko ofisi ya mwanasheria na leo tumeelezwa hivyo tunaomba kujua upelelezi umefikia wapi miongoni mwetu tuna watoto wadogo na kesi yetu haina dhamana,” amedai Ishengoma.

Wakili Magoho alieleza kuwa wapo katika hatua za mwisho kuandaa ripoti wanachosubiri ni taarifa ya hasara iliyotokea ATCL.

Hakimu Kasonde ameahirisha kesi hiyo hadi Juni 3, 2019 itakapotajwa tena.

Mbali na Ishengoma washtakiwa wenginekatika kesi hiyo ni Adamu Kamara, Mlon  Masubo, Alexander Malongo, Tunu Kiluvya, Jobu Mkumbwa, Mohamed Issa, Godfrey Mgomela, Absalom Nyusi na Janeth Lubega.

Pia Soma

Wote wanakabiliwa na mashtaka matatu ikiwemo kujipatiaSh10milioni kwa njia ya udanganyifu kwa lengo la kuwakatia watu tiketi za ndege pamoja na utakatishaji fedha.

Chanzo: mwananchi.co.tz