Kyela. Msafara wa wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Kyela umezuiwa na kundi la vijana waliovalia mashati mekundu.
Vijana hao walipanga mawe na magogo barabarani na kusababisha magari ya viongozi wa kamati hiyo kusimama. Miongoni mwa waliokuwepo katika msafara huo ni mkuu wa Wilaya ya Kyela, Claudia Kitta.
Akizungumza leo Alhamisi 29, 2019 mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Hunter Mwakifuna amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, akibainisha kuwa ilikuwa jana Jumatano Agosti 28, 2019 saa 11 jioni katika kijiji cha Mpuguti kata ya Makwale.
Amesema walikuwa wakitoka kukagua miradi itakayotembelewa na mbio za mwenge wa uhuru wilayani humo Jumatatu Septemba 9, 2019.
Amebainisha kuwa katika tukio hilo watu wawili wamejeruhiwa kwa mawe akiwepo ofisa usalama wa wilaya hiyo na katibu wake.
“Tunashukuru Mungu vyombo vyetu vya usalama vilikuwa makini katika mapambano, gari ya mkuu wa wilaya iligeuzwa na kurudi ilipotoka,” amesema.
Pia Soma
- Wasambaza taarifa za uongo kuhusu madhara ya dawa kushughulikiwa
- Walimu ‘makada wa CCM’ wampiga chenga Dk Bashiru
- Agizo la Majaliwa latekelezwa, kamera zafungwa kituo cha mabasi Moshi