Fri, 5 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa mpira wa kikapu kutokea Marekani Brittney Griner (31) amehukumiwa kifungo cha miaka 9 kwenye jela nchini Urusi kwa makosa ya kukutwa na kusafirisha dawa za kulevya.
Rais Joe Biden wa Marekani amesema kuwa hukumu hiyo "haikubaliki" na ameitaka Urusi kumuachia huru haraka.
Griner alikamatwa Februari 17 mwaka huu katika uwanja wa ndege jijini Moscow, baada ya polisi kusema walikuta makopo yaliyokuwa na bangi kwenye sanduku lake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live