Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkurugenzi Benki M aachiwa huru, atakiwa kulipa mabilioni

79108 Kumar+pic

Tue, 8 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu mkurugenzi mkuu wa Benki M Tanzania, Sanjeev Kumar kulipa fidia ya zaidi ya Sh6 bilioni na faini ya Sh2 milioni baada ya kukiri mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.

Ametakiwa kulipa fidia hiyo ndani ya miezi 24, hadi sasa ameshalipa Sh690 milioni. Kumar ameachiwa huru akitakiwa kulipa kiasi hicho cha fedha kulingana na muda uliowekwa huku Sh2 milioni akiilipa mahakamani hapo leo.

Uamuzi huo umetolewa baada ya upande wa mashtaka  kumfutia mshtakiwa huyo  mashtaka ya uhujumu uchumi na kumsomea mashtaka mawili  ya kuisababishia Serikali hasara na alikiri kuyatenda.

Akisoma adhabu hiyo Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amesema katika mashtaka hayo mawili mshtakiwa atatakiwa kulipa faini ya Sh1 milioni kwa kila kosa.

Amesema pia mshtakiwa atatakiwa kulipa fidia ya zaidi ya Sh6 bilioni katika kipindi cha miezi 24, kila mwezi akipaswa kulipa Sh22.8 milioni

Hakimu Shaidi amesema hati ya kusafiria ya mshtakiwa huyo itabaki katika ofisi za mkurugenzi wa mashtaka nchini (DPP)  na safari zake zote zitafutiliwa na ofisi hiyo.

Pia Soma

Advertisement
Awali, wakili wa Serikali Jaquline Nyantori  amedai  hawana rekodi ya makosa ya nyuma ya mshtakiwa kuomba mahakama kutoa adhabu kulingana na makubaliano ili iwe  fundisho kwake na  wengine

Mshtakiwa huyo anadaiwa Januari 20, 2016  akiwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki M Tanzania kwa vitendo vyake alivyovifanya aliisababishia Serikali kupata hasara ya Sh6 bilioni.

Amesema katika shtaka la pili, mshtakiwa huyo anadaiwa Januari 20, 2016 jijini Dar es Salaam kwa njia ya ulaghai ndani ya Benki M Tanzania akijua ni udanganyifu alijipatia Dola za Marekani 287,000.

Chanzo: mwananchi.co.tz