Dar es Salaam. Veronika Kundya, mke wa mfanyabiashara mwenye asili ya Kenya, Raphael Ongangi amesema mumewe aliachiwa na watekaji karibu na duka la shangazi yake mjini Mombasa , Kenya.
Ongangi alitekwa Oysterbay jijini Dar es Salaam Juni 24, 2019 na kupatikana jana Julai 2, 2019 huko Kenya.
KWa mujibu wa Veronika, mumewe hajui alifikaje eneo hilo ila ajikuta yupo jirani na duka hilo.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Julai 3, 2019
Veronika amesema kwa sasa hawataki kufahamu mengi zaidi ya kumshukuru Mungu baada ya mumewe kupatikana akiwa hai.
“Kikubwa ni kwamba yupo salama, hana majeraha na amesema hakupigwa ila hajui alifikaje karibu na duka hilo la shangazi yake.”
Pia Soma
- Kesi Jamii Forum yapigwa kalenda, upande wa mashtaka wakosa shahidi
- Batuli kumburuza Mwijaku mahakamani
- Mkuchika: Viongozi tatizo mapambano dhidi ya rushwa