Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkazi Tanga akamatwa na gramu 500 za dawa za kulevya

96145 Pic+dawa Mkazi Tanga akamatwa na gramu 500 za dawa za kulevya

Tue, 18 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tanga. Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania (DCEA) imemkamata Hamad Mbaraka kwa tuhuma  za kukutwa na gramu 500 za dawa za kulevya aina ya Heroin.

Mtuhumiwa huyo mkazi wa barabara ya 19 Wilaya ya Tanga mjini  amekamatwa usiku wa kuamkia leo Jumatatu Februari 17, 2020.

Akizungumza leo kaimu Kamishna Jenerali wa DCEA, James Kaji amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa saa 6 usiku, “alikuwa amezificha katika mfuko  mmoja wa plastiki ndani yake kulikuwa na pakiti tatu tofauti zilizokuwa na dawa hizo.”

“Tangu saa 2 usiku jana tulikuwa tunamtafuta mtuhumiwa, tulikuwa tunafanya mawasiliano ila ilipofika saa 6 usiku tulimkamata, kwa sasa yupo mahabusu anaendelea kuhojiwa.”

Amesema wamepeleka kithibitisho hicho kwa mkemia mkuu wa Serikali kwa ajili ya kupimwa.

Amebainisha kuwa katika mahojiano mtuhumiwa huyo amekiri kuwa anapopatiwa dawa hizo huzificha kwenye mashamba eneo la Pangani.

Pia Soma

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz