Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia mhudumu wa baa Pendo Mwakifamba (21) kwa tuhuma za mauaji ya Hilda Mwambona (25) kwa kumkata na chupa sehemu mbalimbali eneo la tumboni.
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia mhudumu wa baa Pendo Mwakifamba (21) kwa tuhuma za mauaji ya Hilda Mwambona (25) kwa kumkata na chupa sehemu mbalimbali eneo la tumboni. Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi Desemba 30, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Urlich Matei amesema tukio hilo limetokea jana wakati mtuhumiwa na marehemu wakigombea Sh2,500 ambayo ni chenji iliyoachwa na mteja aliyekuwa akipata kinywaji.