Sat, 13 Aug 2022
Chanzo: Malunde
Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga linamshikiria Mchungaji wa Kanisa la KKKT -Makedonia ya Lubaga lililopo mjini Shinyanga ambayo ni Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria kwa tuhuma za kumlawiti mtoto mwenye umri wa miaka 8.
Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga ACP Janeth Magomi amethibitisha kukamatwa kwa Mchungaji huyo Agosti 12,2022.
"Tunamshikilia mchungaji (jina limehifadhiwa) kwa ajili ya uchunguzi zaidi na uchunguzi ukikamilika tutamtafikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili", amesema Kamanda Magomi.
Chanzo: Malunde