Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mchuano wa Shahidi na Kibatala kesi ya Mbowe

72298 Shahidipic

Wed, 21 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Shahidi wa sita wa upande wa mashtaka, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa picha alizopiga katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kinondoni, hazionyeshi tarehe na muda uliopigwa.

Ushahidi huo uliochukua saa saba kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi Saa 11:58 jioni.

Kibatala: Picha ulizopiga katika mkutano wa Chadema pale katika viwanja vya Buibui zinaonyesha tarehe na muda uliopigwa?

Shahidi: Hazionyeshi muda wala tarehe.

Kibatala: Tusaidie shahidi cheo cha Koplo ni cha ngapi katika Jeshi la Polisi?

Shahidi: Ni cheo cha tatu, kuna kuruta na constable.

Habari zinazohusiana na hii

Kibatala: Jana (juzi) uliileza mahakama kuwa umemaliza kidato cha nne, ukapata ufaulilu daraja la tatu pointi 24, bado pointi ngapi ufikie division four?

Shahidi: Sijui kwa sababu mifumo ya elimu inabadilika. Baada ya hapo nilienda kusoma Diploma ya Uandishi wa Habari.

Kibatala: Ni mshtakiwa yupi katika video uliochukua katika mkutano ule alitambulisha tarehe ya mkutano?

Shahidi: Sikumbuki.

Soma zaidi gazeti la Mwananchi leo

Chanzo: mwananchi.co.tz