Mon, 6 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa niaba ya wenzake amuomba Jaji Elinaza Luvanda ajitoe kusikiliza kesi yao ili kulinda heshima yake na ya Mahakama.
Wametoa ombi mapema hii leo, wakiwa wamefikishwa katika Mahakama Kuu division ya makosa ya Ufisadi kwa ajili ya kusikiliza makosa yanayowakabili.
Mbowe na wenzake wanashitakiwa kwa makosa ya Ugaidi pamoja na Uhujumu uchumi, na hapo awali walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kabla ya Kesi hii kuhamishiwa katika Mahakama hii yenye Hadhi ya kusikiliza Makosa wanayoshitakiwa nayo kwa mujibu wa taratibu za kimahakama.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live