Tue, 17 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu watatu (majina yanahifadhiwa) kwa tuhuma ya kuiba pikipiki ya mkazi wa kijiji cha Mwamanyiri wilayani Magu mkoani humo, Omary Shaaban (20) ambaye ni dereva bodaboda.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amesema Januari 11 mwaka huu katika kitongoji cha Mwanduru kata ya Bujora wilayani Magu mmoja ya watuhumiwa hao alimkodi dereva bodaboda huyo kabla kumgeuka wakiwa njiani kisha kumnyang'anya pikipiki yake.
Sikiliza kwa makini hapa chini;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live