Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbaroni kwa mauaji ya mke na mwanaye

AMUUA MKE NA MTOTO.jpeg Mbaroni kwa mauaji ya mke na mwanaye

Fri, 15 Jul 2022 Chanzo: BBC Swahili

Wakili mashuhuri wa Marekani ameshtakiwa kwa mauaji ya mkewe na mwanawe, jambo la hivi punde zaidi katika sakata ambayo tayari imemshuhudia Alex Murdaugh akishutumiwa kwa kughushi kifo chake mwenyewe pamoja na makosa kadhaa ya uhalifu.

Maggie Murdaugh, 52, na mwanawe Paul, 22, walipigwa risasi na kuuawa nje ya nyumba yao zaidi ya mwaka mmoja uliopita.

Wakili huyo aliyefedheheka sasa aliripoti kupata miili yao kwenye shamba kubwa la familia huko Carolina Kusini.

‘’Nimeishughulikia sasa,’’ mamlaka inasema Bw Murdaugh aliwaambia wasafirishaji wa polisi katika simu ya 911.

Mzee huyo mwenye umri wa miaka 54 - ambaye tayari yuko jela na anakabiliwa na msururu wa mashtaka ya uhalifu - anakanusha kuhusika na vifo hivyo.

Kulingana na shtaka lililotolewa na baraza kuu la mahakama katika Kaunti ya Colleton ya South Carolina - ambako mauaji yalifanyika - Bw Murdaugh anatuhumiwa kuwaua wawili hao kwa bastola na bunduki.

Pia alishtakiwa kwa makosa mawili ya kupatikana na silaha hatari.

Iwapo atapatikana na hatia, anakabiliwa na kifungo cha miaka 30 jela bila uwezekano wa kuachiliwa huru.

Chini ya sheria za serikali anaweza pia kukabiliwa na adhabu ya kifo.

Chanzo: BBC Swahili