Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbaroni kwa kumbaka binti miaka 10

Abaka Mbaroni kwa kumbaka binti miaka 10

Thu, 14 Jul 2022 Chanzo: BBC

Mwanamume mmoja katika jimbo la Ohio nchini Marekani ameshtakiwa kwa kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 10 ambaye alilazimika kuvuka mipaka ya jimbo kwa ajili ya kutoa mimba baada ya jimbo lake kuzuia utaratibu huo.

Gershon Fuentes, 27, alifikishwa mahakamani huko Columbus siku ya Jumatano.

Masaibu ya msichana ambaye hakutajwa jina yamevuta hisia za kimataifa.

Rais wa Marekani Joe Biden alitoa mfano huo katika Ikulu ya White House alipokuwa akipinga vizuizi vya utoaji mimba, lakini wakosoaji walikuwa wamehoji ikiwa ni uwongo.

Mamilioni ya wanawake na wasichana walipoteza haki ya muda mrefu ya kikatiba ya kutoa mimba baada ya uamuzi wa Mahakama ya Juu ya Marekani mwezi Juni.

Katika hotuba yake Ijumaa iliyopita kulaani uamuzi huo, Rais Biden alitoa ripoti ya kesi ya mtoto huyo, akisema kwa hasira: ‘’Fikiria kuwa msichana huyo mdogo!’’.

Saa chache baada ya uamuzi wa Mahakama ya Juu, wabunge wa Ohio waliharamisha uavyaji mimba baada ya wiki sita, bila ubaguzi wowote kwa waathiriwa wa ubakaji au kulawitiwa.

Mtoto huyo alikuwa na ujauzito wa wiki sita na siku tatu, kulingana na gazeti la Indianapolis Star.

Akirejelewa na daktari wa unyanyasaji wa watoto huko Ohio, msichana huyo alitembelea kliniki huko Indianapolis, Indiana, kuavya mimba mnamo Juni 30.

Ingawa juhudi zinaendelea ili kuzuia ufikiaji wa utoaji mimba katika jimbo jirani la Ohio, utaratibu bado unasalia kuwa halali huko.

Kufuatia uamuzi wa Mahakama ya Juu, majimbo 26 ya Marekani yameweka vikwazo vikali vya utoaji mimba au yanatarajiwa kufanya hivyo katika wiki na miezi ijayo.

Chanzo: BBC