Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mawakili waanza kupambania rufaa ya kina Sabaya

Sabaya2 Pc Data Mawakili waanza kupambania rufaa ya kina Sabaya

Wed, 16 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kesi ya rufaa ya kupinga kifungo cha miaka 30 jela kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili imeanza kusikilizwa leo Februari 15 katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, ambapo Wakili Majura Magafu ametoa hoja 14 akisema kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi haikufanya uchambuzi wa kina wa ushahidi hadi kutoa hukumu hiyo.

Oktoba 15, 2021 Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Arusha ilimkuta na hatia Sabaya na wenzake wawili ya kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na hivyo kuwahukumu kifungo cha miaka 30 jela.

Katika kesi hiyo ya jinai namba 129, inayosikilizwa na Jaji Sedekia Kisanya, waleta rufaa wengine ni Sylvester Nyegu na Daniel Mbura.

Baada ya rufaa hiyo kutajwa mahakamani hapo, Wakili Magafu ameanza kutaja hoja nane, huku akisema hoja nyingine ataendelea nazo Wakili mwenzake Mosses Mahuna.

Amesema kama Hakimu angefanya uchambuzi wa kina angeweza kugundua mambo kadhaa ikiwemo hati ya mashitaka iliyopelekwa mbele yake haikukidhi matakwa ya kisheria na ushahidi uliotolewa ulikuwa hauendani na hati ya mashitaka.

"Mheshimiwa Jaji ground (hoja) ya nane inahusu mheshimwa aliyeendesha hii kesi kufanya uchambuzi wa kina na kuwatia hatiani waleta rufaa na kuwpa adhabu.

“Kwa mujibu wa kifungu cha 312 cha CPA ni matakwa ya kisheria kwamba jaji anapoandika hukumu yake inabidi afanye mchanganuo wa kina juu ya ushahidi ulioletwa mbele yake asipofanya hibyo hiyo hukumu inakuwa ni batili," amesema Wakili Magafu.

Akirejea mashauri ya mahakama ya rufaa ikiamua juu ya suala hilo, Magafu amesema; "Kila hakimu au jaji anayo staili au utaratibu wake wa kuandika hukumu lakini kitu cha msingi anachotakiwa kuangalia ni kupitia viini vyote vya mashitaka na ushahidi kama ulivyotolewa na pande zote."

Wakili Magafu amesema tatizo la kwanza lilikuwa ni kuhusu majina ya washitakiwa mshitakiwa wa kwanza na wa tatu (Sabaya na Mbura) na kwamba, Julai 18, 2021 wakati shauri likiendelea Jamhuri iligundua jina la mshitakiwa wa kwanza lilikuwa limekosewa na wao wakasema ni ‘typping error’ ila wao wakasema hapana na kuhusu jina la mshitakiwa wa tatu ambaye yeye mwenyewe analikana limeendelea kuwepo kwenye hati ya mashitaka.

"Mheshimiwa Jaji wakati maelezo ya hoja ya awali, mshitakiwa wa tatu alikana hilo jina linaloonekana kwenye charge sheet (hati ya mashitaka) ushahidi wa kukana jina uko ukurasa wa nne wa nakala ya hukumu.

“Tatizo lingine ni mahali ambapo tukio lilitokea mashahidi wanasema tukio lilitokea mtaa wa Soko Kuu lakini charge sheet mpaka leo inaonyedha tukio liliyokea mtaa wa Bondeni Arusha," ameeleza Magafu.

Ameendelea; "Mheshimiwa ili charge sheet iweze kuitwa charge sheet lazima ionyeshe kinaga ubaga ni nani alikuwa mlalamikaji kwenye hilo tukio na lilitokea eneo gani na kifungu cha sheria anachoshitakiwa nacho.Baada ya upande wa mashitaka kuona kulikuwa na utata juu ya tukio lilipotokea walijaribu kumuita shahidi wa 11 ili awasaidie kutatua hilo tatizo.”

Wakili huyo amedai kuwa shahidi wa 11 DC James, ushahidi wake kuanzia ukurasa 168 ukiangalia aya ya mwisho anasema alipopewa faili kufanyia uchunguzi alienda Soko Kuu katika duka la Mohamed Saad akini wakati akihojiwa alisema tukio liliyokea Mtaa wa Bondeni Arusha.

Aliendelea kudai kuwa kwa mujibu wa sheria hati inataka itaje walalamikaji kwa majina na kwa mujibu wa hati ile inaonyesha walalamikaji walikuwa watatu ambao ni Bakari Msangi, Ramadhan Ayoub na Saad.

"Nataka nifafanue zaidi mpelelezi ambaye ni PW 11 yeye anasema kwamba mlalamikaji katika shauri hili aliyefika mbele ya polisi ni PW 6, tunashindwa kuelewa shahidi wa kwanza na wa tatu ambao hawajawahi kufika polisi wanakuwaje sehemu ya walalamikaji hii inaonekana kulikuwa na hola katika uandaaji wa mashitaka?

"Hakuna sehemu yoyote katika walalamikaji walioandika kutoka polisi PW 7, Gwakisa Minga hakusema kama aliwahi kuwaita mashahidi namba moja na tatu kwa ajili ya kuwahoji.

"Kwa hiyo tunasema mheshimiwa Hakimu angeweza kufanya upembuzi halali na umakini angegundua kasoro nyingine zote,tukio linadaiwa kutokea sehemu moja lakini katika kuhakikisha washitakiwa wanatiwa hatiani wakatenganisha hizo count zikawa tatu,"

Ameendelea kusenma kuwa upande wa mashitaka walileta kielelezo cha tatu na wakati walipokuwa wakifanya uchunguzi wao walimpiga picha Bakari Msangi wakasema waliipeleka forensic bureau kwa ajili ya kuihakiki.

"Kitu kinachotufanya tuone hicho ni cha kupika kielelezo P5 kinaunga mkono tunachokisema sasa hivi fomu ya polisi namba 27.

“Inaonyesha barua ya kupeleka hizo picha iliandikwa 24/7/2021 wakati kesi inakaribia kuisha hii haukuwa utaratibu sahihi kwani polisi hawawezi kuendelea kufanya upelelezi wakati kesi iko tayati mahakamani inasikilizwa,"alieleza

"Mheshimiwa Jaji kama inavyojua prosecution wanapomaliza upelelezi huiomba mahakama kesi ianze kusikilizwa, hawatakiwi kusikiliza ushahidi unaoendelea mahakamani kisha waende kufanya upelelezi wazibe mapengo. Baada ya kugundua wameshafanya makosa na wanataka wazitumie picha za PW6 ambaye ndiyo mlalamikaji wakaandika barua ya tarehe 26/6/2021 na majibu yakawaumbua," alisema.

Kuhusu wadaiwa PW 2 na 4, alisema licha ya kuwa walikuwa wamenyanyasika sana kwa kupigwa na mshitakiwa lakini waliwaomba wawanulie ndizi.

“Hapo ndiyo utaona kuna shida kwenye upelelezi wa hii kesi na uchambuzi wa ushahidi, mtu aliyekupiga sana huwezi kumuomba akununulie ndizi,” amesema.

"Sisi tunaona mheshimiwa Hakimu hakuweza kujielekeza vizuri katika uchambuzi wa ushahidi ulioletwa mbele yake.Mheshimiwa tuna submit vilevile angeweza kugundua PW 6 ambaye ndiye aliyekuwa chanzo cha hii kesi alikuwa na hila dhidi ya mleta rufaa wa kwanza," amesema.

Akizungumzia suala la upelelezi kutokufanyika vizuri alidai kuwa ameshatoa sababu baadhi ya wapelelezi hawakufanya upelelezi vizuri baada ya kupata malalamiko toka kwa PW 6 na kuwa haiwezekani kwa hali ya kawaida polisi wako kwenye eneo la tukio, haiwezi kusema Bondeni Street na Sokoni street ziko pamoja.

"Polisi wangechunguza vizuri wangejua ni uongo. Pw 6 anasema alipekuliwa akaibiwa 390,000 na simu lakini PW 4 anasema alishuhudia PW6 akipekuliwa alichoshuhudia aliona akinyang'anywa simu na wallet na kama wakati anapekuliwa hawa wengine waliona walipaswa kuona fedha zikichukuliwa hatupaswi kuweka watu hatiani kwa maneno ya kusikia bali ushahidi madhubuti,"

Aliendelea kueleza kuwa waleta rufaa walikanusha wizi wa Sh35,000 na PW 3 alisema alienda pale kwa ajili ya kununua bidhaa kwenda kuuza kwenye ushahidi wake anasema 35,000 alipewa kwa ajili ya kwenda kununua vitu vya nyumbani vya kula mheshimiwa tunajiuliza kwanini hakwenda polisi kulalamika.

Baada ya Wakili Magafu kutoa hoja hizo, Wakili Mahuna naye aliendelea kuwasilisha hoja ambapo alianza na hoja ya rufaa ya kwanza aliyodai kiwa ni Mahakama ya Hakimu Mkasi Arusha ilikosea kuwatia hatiani na kuwapa adhabu waleta rufaa kwani hati ya mashitaka ilikuwa batili.

Alieleza mahakama kuwa na mashitaka matatu yote unyang'anyi wa kutumia silaha yameonekana kuna tatizo bayana la ni wapi tukio hilo lilitendeka hiyo 9/2/2021 na kuwa katika ukurasa wa 112 wa uamuzi wa mahakama ilielezwa hoja za majumuisho za mawakili na mahakama ilisema shahidi wa saba na wa 11 wote wawili walisema duka hilo liko Bondeni street karibu na Soko Kuu.

"Tunajiuliza hilo ni sawa kwenye ukurasa wa 124 Gwakisa anasema kuwa alifahamishwa na mrufani wa kwanza bwana Sabaya kuwa aliwakamata PW2 na PW4 kwenye duka lao huo sokoni.

"Siku ya 12/2/2021 na 12 1 2021 alienda yeye PW 7, 2, 4 kwenye duka la PW 2 na 4 lililoko Bondeni Street lililoko karibu na Soko Kuu. Duka linalozungumziwa hapa ni la PS 1 lililopo bondeni street near market .PW 7 hakuwahi kuzungumzia duka la PW 1 ambalo ndilo lipo kwenye hati ya mashitaka na PW 11 anasema kosa lilitendeka Soko Kuu kwenye duka la PW 1 na hazungumzii chochote juu ya duka lililopo Bondeni," amesema.

Wakili Mahuna alidai tatizo lingine ni tarehe ambapo kwenye hati ya mashitaka inadaiwa 9/2/2021 washitakiwa hao waliiba Sh Milioni 2.769 lakini shahidi wa pili wa jamhuri anasema siku hiyo hakujua nini kiliibiwa dunkani hadi walipofungua duka 12/2/2021.

Baada ya kuwasikiliza mawakili hao, Jaji Kisanya ameahirisha rufaa hiyo hadi kesho mawakili hao watakapoendelea kuwasilisha hoja zao za rufaa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live