Fri, 29 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii maarufu anayetamba kupitia mtansao wa TikTok na kufanikiwa kupata dili kubwa za mamilioni ya fedha nchini India na nchi nyingine nje ya Tanzania, Kili Paul amevamiwa na watu wasiojulikana.
Kupitia Insta story yake, Kill Paul amesema ameshambuliwa na watu watano (5) kwa visu na marungu ambapo ameweza kupambana nao wakakimbia.
Staa huyo ambaye amekuwa akiimba nyimbo za wasanii mbalimbali maarufu na kuziposti kwenye mtandao wa TikToko kwa sasa amelezwa Hospitalini baada ya kushonwa nyuzi tano.
Kili amesema watu hao walitaka kumpoteza lakini Mungu amaemsaidia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live