Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Masauni awataka polisi wawakamate walioua 12 mgogoro wa wakulima na wafugaji

PIX 4 1 1 768x512 Masauni awataka polisi wawakamate walioua 12 mgogoro wa wakulima na wafugaji

Tue, 1 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata mara moja wafugaji waliohusika katika mauaji ya watu 12 Mkoani Lindi.

Masauni ametoa kauli hiyo akiwa ameambatana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi katika Vijiji vya Kikole, Kipindimbi na Zinga Kibaoni Wilayani Kilwa, Mkoani humo Oktoba 31, 2022, katika ziara yao kufuatia mgogoro wa wakulima na Wafugaji mkoani humo.

Alisema Serikali haiwezi kukaa kimya wakati matukio hayo ya kinyama yakiendelea na haitakubali kuona mfugaji au mkulima anavunja sheria, amani, hivyo lazima sheria ifuatwe na atakayekiukwa atashughulikiwa.

“Natoa maelekezo kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha watu wote nchi nzima walioshiriki kuua watu wengine, ikiwemo hawa walioua wakulima katika Wilaya hii ya Kilwa na Wilaya zingine za Mkoa huu wa Lindi ambazo tunakwenda kwanza wakamtwe, ninashangaa mpaka leo hakuna mtu hata mmoja aliyekamatwa, inatutia mashaka makubwa,” alisema Masauni na kuongeza;

“Kamishna upo hapa na RPC upo hapa hakikisheni hawa mnawakamata haraka ili iwe fundisho kwa watu wengine, haiwezekani mtu anaua raia kama anaua kuku, watu 12 wamekufa katika mkoa huu wa Lindi, hawa ni binadamu, leo ameua mmoja akamatwi, kesho kaua mwingime hakamtwi, naa hata waliofanya uhalifu kuiba au kujeruhi nao wakamatwe.”

Aliongeza kuwa kwa yeyote ambaye ameshiriki katika kusababisha matatizo hayo ya vifo katika kutenda makusudi au kuzembea, kwa wale ambao wanaihusu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na wengine ametaka kila mtu awajibike kwa nafasi yake na kila ambaye yupo chini ya Serikali kwa ujumla wake anataka wawajibike ipasavyo.

Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka wafugaji waliopo katika vijiji ambavyo hawaruhusiwi kuwepo, waondoke katika maeneo hayo, waende katika vijiji vilivyopangwa kwa ajili ya mifugo.

“Nawataka wafugaji kuacha tabia ya kupeleka mifugo katika mashamba ya wakulima, marufuku kupeleka mifugo yenu katika maeneo ambayo hamruhusiwi ikiwemo katika Kijiji hiki cha Kikole, lazima utaratibu ufuatwe,” alisema Ndaki.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live