Mwanamume mmoja ameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi waliomvamia usiku katika daka lake katika katika soko la Khayega eneo bunge la Shinyalu kaunti ya Kakamega.
Majambazi Wampiga Risasi na Kumuua Mhudumu wa M-Pesa kwa Kuchelewa Kuwapa Pesa Mwanamume huyo aliuawa kwa kupigwa risasi na majambazi. Chanzo: UGC Majambazi watatu waliojihami kwa silaha kali walimvamia Kevin Orata katika duka lake la M-Pesa usiku wa Jumatatu - Disemba 26 na kutekeleza unyama huo.
Akithibitisha kisa hicho Kamanda wa Polisi wa Kaunti Ndogo ya Kakamega Mashariki Robert Makau alisema kuwa Orata aliyekuwa na umri wa miaka 23 alipigwa risasi na kuaga dunia papo hapo.