Wed, 14 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imetupilia mbali pingamizi lililowekwa na mawakili wa utetezi katika kesi ya rufaa iliyofunguliwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake watano.
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Desemba 14, 2022 na Jaji Salma Maghimbi ambaye anasikiliza shauri hilo, baada ya jana kusikiliza hoja za pande zote mbili.
Jana mawakili wa Sabaya na wenzake watano wameweka pingamizi la awali katika kesi ya rufaa waliyofunguliwa na Serikali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live