Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama yataka majibu ya kutosha kesi ya askari JWTZ

77113 Mahakama+pic

Wed, 25 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam nchini Tanzania imesema kesi  inayomkabili Ramadhan Mlaku ambaye ni Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) itakapokuja tena  mahakamani hapo upande wa mashtaka wawe na majibu ya kutosha kwa kuwa shauri hilo lipo zaidi ya  mwaka mmoja na upelelezi bado haujakamilika.

Hatua hiyo imekuja baada ya Wakili wa Serikali, Candid Nasua kudai leo Jumanne Septemba 24, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa jalada halisi lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kupitiwa na kutolewa uamuzi.

Simba amesema tarehe ijayo shauri hilo lisipokuja mahakamani hapo upande wa mashtaka waeleze upelelezi umefikia kwenye hatua gani.

"Upelelezi umechukua muda mrefu hadi sasa ni mwaka mmoja na nusu, siyo rahisi kuahirisha bila ya kuwa na maelezo ya kutosha, nakuagiza ukawaambie nataka majibu shauri hilo litakapokuja tena," amesema Simba.

Shauri hilo limeahirishwa hadi Oktoba 8, 2019 litakapokuja kwa ajili ya kutajwa.

Kwa Mara ya kwanza shauri hili lilifikishwa mahakamani hapo Machi 14, 2018 ambapo mshtakiwa huyo anakabiliwa na shtaka la mauaji.

Pia Soma

Advertisement
Inadaiwa mshtakiwa huyo ambaye ni Mwanajeshi wa Kambi ya Makongo alitenda kosa hilo Oktoba 30, 2017 akiwa Makao Mkuu ya JWTZ Upanga Ilala Dar es Salaam ambapo alimuua askari mwenzie MT 79512 SGT Munyama.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz