Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama Kuu Tanzania yafuta hukumu iliyowafunga waandishi wa habari

68125 Mahakama+pic

Wed, 24 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mwanza. Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza leo Jumatano Julai 24, 2019  imefuta mwenendo mzima wa kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela waliyopewa watu wa tatu wakiwemo waandishi wa habari wawili.

Pamoja na kufuta mwenendo wa kesi na hukumu, Mahakama pia imeagiza shauri hilo lisikilizwe upya mbele ya Hakimu mwingine.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji Mohammed Siani baada ya kukubaliana na rufaa iliyokatwa na waandishi wa habari,  Christopher Gamaina na Zephania Mandia na mwenzao Manga Misalaba.

Jaji Siani pia ameagiza usikilizaji upya wa kesi hiyo uzingatie sheria, kanuni, taratibu na haki ya pande zote mbili.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya hukumu hiyo, wakili wa washitakiwa hao, Constatine Mutalemwa ameishukuru mahakama kwa kutenda haki na kuahidi kukamilisha taratibu za kisheria kuwezesha shauri hili kuanza kusikilizwa upya ili wateja wake watendewe haki.

Waandishi hao pamoja na mwenzao tayari wamekaa gerezani kwa miezi mitatu hadi kufikia leo tangu walipohukumiwa.

Pia Soma

Katika shauri 11/2018 iliyosikilizwa na kuamuliwa mbele ya Mahakama ya Hakimu mkazi wilaya ya Magu, mkoani Mwanza waandishi hao na wenzao wawili walidaiwa kutumia nguvu kupora fedha.

Miongoni mwa hoja za rufaa namba 70/2019 zilizokubaliwa na Mahakama ni pamoja na Hakimu aliyesikiliza na kuamua shauri kutozingatia sheria wakati wa ushahidi na baadhi ya mashahidi kutotia saini maelezo yao yaliyotumika kama ushahidi mahakamani.

Chanzo: mwananchi.co.tz