Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Madini ya Sh1.3 bilioni yakamatwa Tanzania

65390 Pic+madini

Thu, 4 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Idara ya Ukaguzi na Udhibiti wa Utoroshwaji  Madini  katika mpaka wa Namanga mkoani Arusha nchini Tanzania imekamata madini  yenye thamani ya Sh1.3 bilioni mwaka kuanzia mwaka 2018 hadi sasa.

Ofisa mfawidhi wa idara hiyo, Arnold  Kishashu ametoa taarifa hiyo leo Jumatano Julai 3, 2019 katika kikao cha tathmini ya utendaji kazi wa taasisi 14 za Serikali zinazo fanya kazi katika kituo cha pamoja cha forodha.

Amesema madini hayo yenye uzito wa kilo 63.645  yamekamatwa  mwaka 2018/2019.

Akizungumza baada ya taarifa hiyo, mkuu wa Wilaya ya  Longido, Frank Mwaisumbe ameeleza kuridhishwa na utendaji wa idara hiyo na kuagiza Mamlaka ya Mapato Namanga kuwapa ofisi katika jengo lao.

Chanzo: mwananchi.co.tz