Wed, 2 Aug 2023
Chanzo: Jamii
Maafisa watatu wa Ushirika wanadaiwa kutumia gari la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu kufanya uhalifu katika Ofisi za Vyama vya Kilimo na Masoko (AMCOS) na kukusanya Tsh. Milioni 2.5 katika ofisi 2, waliposhtukiwa wakakimbia na kutelekeza gari Bariadi.
Alipotafutwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge kuhusiana na tuhuma hizi, ambaye amesema;
“Ni tukio la kweli, mtuhumiwa Mustafa Kimomwe anashikiliwa, wawili wamekimbia na wanaendelea kutafutwa, madai kuwa walikuwa na bastola hilo tumeambiwa lakini hatujui kama ni ya kweli au bandia kwa kuwa hatujaiona.”
Chanzo: Jamii