Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maafisa wa serikali wasimamishwa kazi kwa tuhuma zinazohusu wakimbizi

3009 Refugees E1466416279591 600x400

Mon, 12 Feb 2018 Chanzo: millardayo.com

Taarifa kutoka Uganda ni kwamba Maafisa wanne wa Serikali ya Uganda hivi karibuni wamesimamishwa kazi kutokana na madai ya kutoa takwimu za uongo juu ya wakimbizi wa nchini humo.

Uchunguzi juu ya wafanyakazi hao unaendelea, mmoja kati yao akiwa ni Kamishna wa Wakimbizi nchini humo Apollo Kazungu na uchunguzi huu pia utaangalia kama viongozi wa mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa walihusika.

Inaelezwa kuwa wafanyakazi hao walizidisha takwimu za idadi ya wakimbizi hao. Inasemekana kuwa Uganda ilichukua wakimbizi hadi milioni 1.4 kutoka Sudan Kusini na DRC ikiwa ni idadi ya juu zaidi kuliko nchi yoyote kwa mwaka 2016.

Alichozungumza Kibatala baada ya Sugu kuachiwa, ametaja kilichokuwa kinakwamisha dhamana

TATU MZUKA: Kitu amefanya Mshindi wa Mil 22 baada ya Kuipokea pesa yake



Chanzo: millardayo.com