Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MAUAJI YA MWANAFUNZI SCOLASTICA: Aliyehukumiwa kunyongwa mauaji Scolastica akata rufaa

62058 SCOLASTICA+PIC

Tue, 11 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi. Aliyekuwa mshtakiwa wa kwanza, Hamis Chacha katika kesi ya mauaji ya mwanafunzi wa Scolastica, Humphrey Makundi (16), ameamua kukimbilia Mahakama ya Rufaa kupinga hukumu ya kifo.

Juni 3, Jaji Firmin Matogolo wa Mahakama Kuu, alimhukumu Chacha kunyongwa hadi kufa, huku washtakiwa wenzake wawili wakihukumiwa kifungo cha miaka minne jela kila mmoja.

Mbali ya Chacha ambaye alikuwa mlinzi wa shule hiyo wengine ni mmiliki wa shule, Edward Shayo maarufu “Kingsize” na mwalimu wa nidhamu wa shuleni hapo, Laban Nabiswa.

Mwanafunzi huyo aliuawa usiku wa Novemba 6, 2017 kwa kupigwa mapanga na Chacha na baadaye akawaita kwa simu Shayo na Nabiswa ambao baada ya kufika, Shayo aliagiza mwili utupwe mtoni.

Akizungumza jana na Mwananchi, wakili aliyekuwa akimtetea Chacha, David Shillatu alisema leo atawasilisha notisi ya kukata rufaa kupinga mambo mawili; hukumu pamoja na adhabu aliyopewa mteja wake.

“Nitawasilisha notisi kesho (leo) kisha nikipewa tu records (kumbukumbu) za Mahakama nitaandaa sababu za rufaa na kuziwasilisha Mahakama ya Rufaa halafu tutasubiri taratibu zingine,” alisema.

Habari zinazohusiana na hii

Aidha, wakili Elikunda Kipoko aliyekuwa akimtetea Shayo alisema ni mapema kusema watachukua hatua gani baada ya hukumu ya mteja wake.

Wakili Patrick Paul aliyemtetea Nabiswa ambaye ni raia wa Kenya, alisema suala la kukata rufaa ni la mteja na bado alikuwa hajapata maelekezo hayo.

Chanzo: mwananchi.co.tz