MAADHIMISHO ya siku ya Kimataifa ya Kupambana na Rushwa na Siku ya Kimataifa ya haki za Binadamu yatafanyika jijini Dodoma kesho.
Kaulimbiu ya maadhimisho kwa mwaka huu ni 'Uzingatiaji wa Ahadi ya Uadilifu kwa Viognozi na Watumishi kwa Ustawi wa Utawala Bora na Haki za Binadamu nchini'
Maadhimisho ya mwaka huu yatashirikisha wadau wa sekta ya umma na sekta binafasi, taasisi zizizo za kiserikali pamoja na wabia wa maendeleo .
“ Tumejipanga kukumbushana juu ya umuhimu wa kuzingatia misingi ya ahadi ya uadilifu ambao ndio mwongozo wa mwenendo wa watumishi waliopewa dhamana ya kuwahudumia wananchi katika sekta ya umma na binafasi,” amesema Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni Mstaafu George Mkuchika.