Wed, 4 Aug 2021
Chanzo: Mwananchi
Mahakama ya Wilaya ya Temeke leo Jumatano Agosti 4, imemuhukumu mkazi wa Mtongani jijini Dar es Salaam, Joakim Komba maarufu Domo la Mbwa au Pilato (21) kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kuiba kiasi cha Sh, 880,000 na simu yenye thamani ya Sh. 350,000.
Pia mahakama hiyo imeamuru mshtakiwa huyo kuchapwa viboko 10 kabla ya kuanza kutumikia kifungo hicho.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Jimson Mwankenja akisema mahakama hiyo imezingatia adhabu iliyoanishwa katika kifungu cha 227A ya kanuni ya adhabu unyang'anyi wa kutumia silaha haitakiwi kuwa chini ya miaka 30 jela.
Chanzo: Mwananchi