Thu, 31 May 2018
Chanzo: bongo5.com
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC), kimekanusha taarifa ya kuwa Bi Hellen Kijo Bisimba ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Wazee Chadema.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)inaukumbusha umma wa watanzania kuwa Dkt. Helen Kijo-Bisimba bado ni Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC mpaka Juni 30, 2018.
LHRC kupitia ukurasa wake wa Twitter wameandika hivi: Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinakanusha taarifa hii na kuukumbusha umma wa watanzania kuwa Dkt. Helen Kijo-Bisimba bado ni Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC mpaka Juni 30, 2018.Taarifa iliyoelezwa ni ya kupuuzwa ni hii hapa chini:
Taarifa hii ni uzushi na ni ya kupuuzwa.
Loading...
Chanzo: bongo5.com