Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kizimbani kwa kukutwa na ubongo wa fisi

69424 Ubongo+pi

Fri, 2 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wakazi wawili wa mkoani Morogoro  wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matano ya kukutwa na nyara za Serikali, ukiwemo ubongo wa fisi.

Wakili wa Serikali Tully Helela amewataja washtakiwa hao kuwa ni Salum Kaluona (65) na Juma Kigombalima (43).

Akiwasomea  mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi,  Augustina Mmbando leo Alhamisi Agosti Mosi, 2019,  Helela amedai washtakiwa hao wametenda kosa hilo Julai 11, 2019 eneo la Buguruni, Dar es Salaam.

Amesema wamekutwa na nyara hizo zenye thamani ya Sh27.2milioni.

Katika shtaka la kwanza, Helela amedai siku na eneo hilo, washtakiwa walikutwa na mikia mitano ya nyumbu, shtaka la pili ni kukutwa na pua mbili, mikia miwili na ubongo wa fisi.

Iliendelea kudaiwa mahakamani hapo kuwa katika shtaka la tatu, siku na eneo hilo la Buguruni, washtakiwa walikutwa na koromeo moja na kipande kimoja cha ngozi ya simba.

Pia Soma

Shtaka la nne na la tano, washtakiwa hao wanadaiwa kukutwa na ndege mbalawaji na kucha nane za ndege Muhanga.

Hata hivyo, upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi bado haujakamilia na kuiomba mahakama kupanga  tarehe nyingine kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa.

Hakimu Mmbando ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 13, 2019  huku washtakiwa wakirudishwa rumande kutokana na mashtaka yanayowakabili kutokuwa na dhamana.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz