Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kilo 700 za mirungi zakamatwa

10754 Mirungi+pic TanzaniaWeb

Wed, 8 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi. Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro kwa kushirikiana na kikosi maalum cha kuzuia Magendo cha Mamlaka ya mapato nchini (TRA) wamekamata zaidi ya kilogramu 700 za mirungi zinazodhaniwa kutokea nchi jirani ya Kenya.

Akizungumza jana Agosti 7 na waandishi wa Habari mkoani hapa Kamanda wa Jeshi la Polisi  Kilmanjaro, Hamis Issah amesema gari hilo lilionekana asubuhi katika barabara ya Arusha-Moshi.

Amesema kikosi maalum cha polisi kwa kushirikiana na TRA walilitilia shaka gari ambalo lilionekana limebeba mzigo mkubwa na kulifuatilia.

“Baadaye gari hilo baadaye lilitelekezwa karibu na daraja la Karanga mjini Moshi,” amesema.

Kamanda Issah  amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa gari hilo ni la nchi jirani ya Kenya.

Kamanda Issa alisema kuwa wanamtafuta  mmiliki wa gari hilo ili kujua ni nani aliyehusika na usafirishaji huo wa mirungi ili kuchukua hatua kali za kisheria na kumpeleka kwenye vyombo husika.

“Tunawaambia wananchi kuwa tumejipanga na matukio kama haya tunahakikisha wale wote waliojihusisha na biashara hii tunawakamata na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kwani tukio hili ni la jinai,”amesema Kamanda Issah.

 Kwa upande wake,  Meneja wa  TRA,Mkoa wa Kilimanjaro Msafiri Mbibo amesema  kikosi chao maalum cha kuzuia magendo (fast team) kililitilia shaka gari hilo ndipo wakalifuatilia ili kujua limebeba  mzigo gani lakini baada ya  mhusika kujua gari hilo linafuatiliwa alikimbia.

“Tulilikamata gari hilo likiwa na mzigo mkubwa wa mirungi  na tulipima uzito wa mirungi hiyo  tukapata una zaidi ya kilo  700 pamoja na vitu vingine ambavyo vilikua kwenye gari,ni pamoja na vitambulisho vyenye usajili wa gari hilo,funguo  ambavyo vitatusaidia  kumpata mhusika kirahisi,”amesema Mbibo.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz