Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kijana anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja akatwa kichwa

Ahmad Abu Marhia Ahmad Abu Marhia

Fri, 7 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Polisi wa Palestina wamemkamata mshukiwa wa mauaji ya mwanaume mwenye umri wa miaka 25-baada ya mwili wake kupatikana ukiwa umekatwa kichwa katika eneo lililovamiwa la Ukingo wa Magharibi.

Makundi ya watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja -LGBTQ nchini Israel, ambako Ahmad Abu Marhia alikuwa meomba ukimbizi, yanasema alikuwa amepokea vitisho kwasbabu ya kuwa mtu anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Video ya tukio la mauaji hayo yaliyofanyika Hebron ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii na kuibua tetesi kuhusu sababu ya mauaji yake, lakini polisi haijathibitisha lolote.

Haijawa wazi kwa sasa ni kwa jinsi gani Bw Abu Marhia aliishia kwenda hadi katika mji huo ambako alikuwa ametoroka awali.

Makundi ya LGBTQ yanasema kuwa alikuwa ameishi miaka miwili nchini Israeli akisubiri kuomba ukimbizi akidai kuwa alitoroka Ukingo wa Magharibi baada ya kupokea vitisho kutoka kwa jamii yake.

Vyombo vya habari vya Israeli vimewanukuu marafiki zake wakisema alitekwa na kupelekwa Ukingo wa Magharibi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live