Dar es Salaam. Mahakama ya Wilaya ya Ilala Agosti 29, 2019 itaanza kuisikiliza kesi ya kuvunja, kuiba na kubakwa kwa mtoto wa miaka 15 inayowakabili washtakiwa, Omary Mussa (30) na Maulid Juma (20).
Wakili wa Serikali, Anna Chimpae mwishoni mwa wiki iliyopita amedai mbele ya Hakimu Mkazi, Adolf Sachore kuwa katika usikilizwaji wa kesi hiyo upande wa mashtaka wanatarajia kuwaita mashahidi saba kutoa ushahidi katika kesi hiyo.
Hatua hiyo ilifikiwa mahakamani hapo baada ya upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo na washtakiwa hao kusomewa maelezo ya awali.
Akiwasomea maelezo hayo, Chimpae amedai Juni 26, 2018 eneo la Pugu Kajiungeni washtakiwa walivunja nyumba ya Elizabeth Zacharia na kutenda kosa.
Chimpae amedai mbali na kuvunja nyumba hiyo, washtakiwa hao waliiba simu mbili aina ya Tecno na zenye thamani ya Sh480,000 na fedha taslimu Sh20,000
mali ya Elizabeth Zacharia.
Pia Soma
- Jinsi moto ulivyomfuata aliyekimbilia juu ya mti
- Migogoro ya ardhi, mfumo dume vyatajwa kuwa kero wananchi wa Korogwe, Lushoto
- Mwanafunzi ajiua kwa kujipiga risasi
Washtakiwa hao walikubali maelezo yao binafsi ikiwemo majina yao, shughuli zao na wanapoishi na kuyakana mashtaka yanayowakabili.