Kesi ya uhujumu uchumi namba 27/2021 inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na wenzake sita imeahirishwa katika mahakama ya hakimu mkazi arusha kutokana na nyaraka zinazoiwezesha mahakama hiyo kuendesha shauri hilo kutokukamilika.
Kwenye kesi hiyo Sabaya na wenzake Sita wanakabiliwa na Mashtaka manne huku mawili yakimkabili Sabaya peke yake.
Hakimu Patricia Kisinda aliyesikiliza shauri hilo ameahirisha kesi hiyo hadi September 9/2021
Mashtaka manne kwenye kesi hiyo ni Kuongoza genge la uhalifu, Uhujumu uchumi, Rushwa, na kujipatia fedha kinyume cha sheria makosa ambayo wanadaiwa kuyatenda mwaka huu eneo la Morombo jijini Arusha.