Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kesi ya Sabaya: Pingamizi la Jamuhuri lapigwa chini

Sabaya 2?fit=680%2C453&ssl=1 Aliekuwa Mkuu wa Wilaya wa Hai Lengai Ole Sabaya

Wed, 4 Aug 2021 Chanzo: global publishers

Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imeondoa pingamizi la upande wa Jamhuri lililowasilishwa mahakamani hapo kupinga upande wa utetezi kumhoji shahidi namba sita wa upande wa Jamhuri kuhusu maelezo aliyoyatoa polisi katika kesi ya jinai namba 105 ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili.

Akitoa uamuzi huo mdogo, Hakimu Mwandamizi anayeendesha shauri hilo, Odira Amworo amesema baada ya kufuatilia vifungu vya sheriana kurejea kesi nyingine zilizopita, amebaini kuwa hakuna mwongozo unaoweka wazi sheria kuzuia mahojiano kama hayo.

Hapo juzi, Agosti 2, 2021, mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi la wakili wa utetezi, Sylvester Kahunduka la kuomba kumhoji shahidi wa sita katika kesi hiyo Bakari Msangi ambaye anaonekana kutokumbuka maelezo aliyoandika polisi.

Chanzo: global publishers