Fri, 6 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeipiga kalenda kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikael Mbowe hadi Agosti 13 2021.
Mahakama imefikia hatua hiyo mara baada ya upande wa mashtaka kudai taratibu za kuifungua kesi hiyo katika Mahakama yenye mamlaka ya kuisikiliza hazijakamilika
Mbowe alifikishwa Mahakamani hapo Julai 26 mwaka huu, aliposomewa mashtaka yanaymkabili ikiwemo kupanga njama za kuwaua viongozi wa kisiasa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live