Mon, 23 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kesi ya Ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikale Mbowe na wenzake watatu,imefungwa rasmi Mahakamaya Hakimu Kisutu na kuhamishiwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa.
Uamuzi huo umetolewa leo na Hkimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba mara baada ya washtakiwa kusomewa maelezo ya mashahidi na vielelezo.
Hata hivyo upande wa mastaka unatarajia kiuwa na mashahidi 24 na vielelezo 19 kuthibitisha mashtaka dhidi ya washitakiwa hao.
Awali kesi hiyo ilipokea mapingamizi yaliyotaka usikilizwaji ufanyike katika Mahakama yenye hadhi ya kusikiliza kesi za Ugaidi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live