Mon, 23 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mashahidi 24 na vielelezo 19 wanatarajia kutoa ushahidi katika kesi ya Ugaidi inayomkabili, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watatu
Miongoni mwa mashahidi hao, yupo aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Boaz
Hayo yameelezwa leo, Agosti 23, 2021 na upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga akisaidiana na Ester Martin, wakati wakiwasomea maelezo ya mashaidi na vielelezo( Commital Proceedings) washtakiwa hao, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba
Chanzo: www.tanzaniaweb.live