Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kesi vigogo TRL yakwama

60141 Pic+tra

Thu, 30 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeshindwa kuendelea kusikiliza kesi inayowakabili vigogo 11 wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) baada ya wakili wa utetezi kuomba muda kupitia jalada.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya madaraka kwa kukiuka sheria wakati wa ununuzi wa mabehewa 25.

Wakili wa utetezi, Tibita Muganga amedai leo Jumanne Mei 28, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Maghela Ndimbo kueleza kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya usikilizwaji na shahidi yupo.

"Kati shauri hili nashiriki kwa mara ya kwanza baada ya wakili, Malamsha aliyekuwepo awali kujitoa nimeshaanza kazi ya kulipitia jalada ninaomba nipewe muda kidogo kwa ajili ya kumalizia kazi hiyo,” amedai wakili Muganga.

Hakimu Shahidi amekubali ombi hilo na kupanga shauri hilo kusikilizwa Mei 29, 2019 na washtakiwa wapo nje kwa dhamana.

Vigogo hao ni aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa TRL, Kipallo Kisamfu; mkuu wa kitengo cha makenika na mhasibu mkuu, Jasper Kisiraga; kaimu meneja wa usafiri, Mathias Massae; kaimu mhandisi wa ufundi na meneja ujenzi, Muungano Kaupunda na mkuu wa ufundi na meneja ujenzi, Ngoso Ngosomwiles.

Pia Soma

Wengine ni mhandisi mkuu wa ufundi, Paschal Mafikiri;  mhandisi mipango,  Kedmo Mapunda;  kaimu mhandisi wa mawasiliano, Felix Kashaingili; mkuu wa usafiri wa reli, Lowland Simtengu; mkuu wa ubunifu na utengenezaji wa nyaraka, Joseph Syaizyagi na kaimu mkuu wa usafirishaji, Charles Ndenge.

Katika hati ya mashtaka inadaiwa kuwa kati ya Februari Mosi,  2013 na Juni 30, 2014 makao makuu ya TRL, Kisamfu akiwa mfanyakazi wa mamlaka hiyo, alitumia vibaya madaraka yake kwa kushindwa kusimamia vizuri zabuni kama ilivyokuwa inatakiwa kwenye vigezo na masharti.

Inadaiwa kuwa tukio hilo ni kinyume cha sheria namba 21 ya manunuzi ya 2004 jambo lililoipa faida kampuni ya M/S Hindusthan Engineering and Industries Limited.

Upande wa Jamhuri ulidai kuwa kati ya Julai Mosi na Agosti 31, 2013, Mafikiri alitumia madaraka yake vibaya kwa kuidhinisha michoro iliyoandaliwa na M/S Hindusthan jambo ambalo ni kinyume cha vigezo na masharti ya zabuni.

Pia, Kaupunda anadaiwa alitumia madaraka vibaya kwa kuruhusu kutengenezwa kwa mabehewa 25 bila kuzingatia vigezo na masharti ya zabuni hiyo.

Katika mashitaka mengine, Kisiraga na Massae wanadaiwa Agosti 5, 2014, walitumia madaraka vibaya kwa kuidhinisha malipo ya Dola 1.3milioni za Marekani bila kuthibitisha matumizi ya mabehewa 25, kupitia cheti cha ukaguzi na cha kukubali kinachotolewa na TRL baada ya kufanyiwa majaribio jambo ambalo ni kinyume cha sheria na kanuni za manunuzi.

Inadaiwa kati ya Januari Mosi na Februari 2014, washtakiwa Kaupunda, Mapunda, Kashaigili, Simtengu na Syaizyagi, wakiwa wajumbe wa bodi ya zabuni, walitumia madaraka yao vibaya kwa kuiruhusu M/S Hindusthan kushinda, ambayo ilikuwa haijakidhi vigezo kushinda zabuni hiyo.

Chanzo: mwananchi.co.tz