Tue, 31 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kanisa Katoliki Jimbo la Kigoma limefungua shtaka katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma kutokana na Mgogoro wa Ardhi yenye ukubwa wa Ekari 39.6
Mashtaka yanawahusu Bodi ya Wadhamini wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halmashauri ya Uvinza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakidaiwa kuchukua eneo la Kanisa ambalo wanalimiliki tangu Mwaka 1920
Washtakiwa wamepanga kujenga Madarasa ya Shule ya Sekondari ya Chumvi bila ridhaa ya Kanisa. Mahakama imepanga shauri litajwe Februari 15, 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live